Saturday, January 31, 2015

MUGABE ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA WA AU


Rais Mugabe 
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa umoja wa Afrika Au kwenye mkutano unaoendelea mjini Addis Ababa Ethiopia
Wajumbe walimteuwa Rais Mugabe mwenye umri wa miaka tisini kwa kauli moja katika mkutano huo na kumtakia mema kwenye harakati mbalimbali za kuimarisha uchumi wa bara la Afrika.
Mugabe amechukua nafasi hiyo ya Uenyekiti kuziba nafasi inayoachwa na Rais wa Afrika Kusini Nkosazana Dlamini-Zuma.
Wadadisi wa masuala ya kisiasa wametilia shaka uteuzi huo wa Rais Mugabe kuongoza  Zaidi ya nchi arobaini ambazi ni wanachama wa umoja huo wakieleza kuwa Mwenyekiti huyo mpya hana mahusiano mazuri mataifa ya Magharibi
Shaka hiyo dhidi ya Mugabe pia imejadiliwa na wanasiasa kuwa pengine ikiwa chachu ya maendeleo kwa Afrika kwa kujitawala yenyewe bila kutegemea nchi wafadhili.


 MAKALLA AKAGUA UJENZI WA BWAWA KUBWA LA MAJO CHOLE, WILAYANI KISARAWE


 Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla (katikati), akizungumza baada ya kukagua bwawa la kuhifadhia maji ya mvua kwa ajili ya matumizi ya wananchi wa vijiji vya Chole na Kwala, wilayani Kisarawe mkoani Pwani leo. Bwawa hilo linalotarajia Bwawa  limejengwa kwa gharama ya sh. Bilioni 1.5, linawezo wa kutoa lita milioni 250 kwa mwaka. Kushoto kwake ni Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Selemani Jaffo



Makalla akikagua ujenzi wa bwawa hilo la Chole


Bwawa la Chole linalojengwa na kampuni ya kitanzania ya Kika


Makalla akiwa na Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Seleman Jaffo baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa tanki la maji katika Kijiji cha Chole, wilayani Kisarawe.




Makalla akimtwisha ndoo ya maji Zena Mwinyihija baada ya kuzindua kisima cha maji katika Kijiji cha Mengo, wilayani Kisarawe.




Makalla akiwa na Mbunge wa Jimbo la Kisarawe, Seleman Jaffo baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa tanki la maji katika Kijiji cha Chole, wilayani Kisarawe.



Wananchi wakisikiliza kwa makini wakati Makalla akihutubia baada ya kuweka jiwe la msingi ujenzi wa Tanki la maji katika Kijiji cha Chole.






Katibu wa Bodi ya Maji ya Kijiji cha Chakenge, wilayani Kisarawe, Pwani, Fatuma Chambuso akisoma taarifa ya usimamizi wa mradi wa maji uliozinduliwa na Naibu Waziri wa Maji katika Kijiji hicho 
Mwenyekiti wa Kijiji cha Chakenge, Mohamed Ndege akimkabidhi zawadi ya mbuzi Naibu Waziri Makalla.




Wananchi wa Kijiji cha Chakenge, wilayani Kisarawe wakicheza muziki wa Mwanamuziki Naseeb Abdul 'Diamond Platinamuz' kufurahia kuzinduliwa kwa mradi wa maji uliofanywa na Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla.

Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla (kulia) akiungana na wananchi kucheza muziki mpya mdogo mdogo wa Mwanamuziki Diamond, baada ya kuzindua mradi wa maji katika Kijiji cha Chakenge, wilayani Kisarawe, Pwani. PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA WA KAMANDA WA MATUKIO BLOG   August 01, 2014


DC in Coast Region cautions over illegal logging in Ruvu South forest

Kisarawe District commissioner, Fatuma Kimario
Kisarawe District commissioner Fatuma Kimario has warned members of natural resource committees in the villages within the district to stop engaging in illegal logging, timber harvesting and charcoal production in the Ruvu South Forest reserve.
 
She said it is very shocking to see and hear that the “watchdogs” of the forest reserve are the same people setting back the district’s move to protect and manage the reserve.
 
The DC gave the warning in Kisarawe during a meeting of sharing of survey results for Ruvu South forest reserve conducted by Tanzania Forest Conservation Group (TFCG) in collaboration with Community Forest Conservation Network of Tanzania (Mjumita).
 
She directed the villages to make sure that they appoint well disciplined and patriotic members who have public interest at heart.
 
“If you go into the forest reserve today, you may shed tears on how the forest reserve has been degraded! I have the evidence that some of you members of this natural resource committee are doing this illegal business,” she said.
 
I think the government should work out plans to invite investors who would invest in animal zoo. I think this would be the best strategy of protecting our forest reserves because they will make sure that they protect these zoos and prevent these illegal loggers,” he said.
 
In another development, the DC advised the government to make sure that it subsidizes gas so that many ordinary Tanzanians who use charcoal and fire wood as their main source of energy can afford to ease pressure on the forest reserves.
 
Kibaha District forest manager, Fortunata Senya said that experience shows that some village natural resource committee members are not trusted at all when it comes to protecting the forest reserve.
 
“Sometimes these people are not trusted. They may give you full support today to arrest the illegal loggers and charcoal producers but immediately when you leave the forest reserve, they start colluding with other illegal loggers to facilitate the ill-gotten gains,” she said.
 
For their part, committee members, Subira Juma and Latifa Feli from Soga, Kibaha, told participants that some unfaithful government officials were in cahoots with a syndicate of powerful business tycoons to mow down the forest reserve.
 
The Members vowed to take to task any government official or village natural resource member who would be found colluding with the charcoal producers.
 
“I was born once and will die once! I don’t fear anything. I will work around the clock to make sure that any member arrested is taken to court immediately,” said Subira amid applause from the participants.
 
Earlier, presenting the research findings, the project manager, Elinas Monga and the forest condition and monitoring officer Justine Gwegime said the illegal logging and charcoal production activities have threatened disappearance of a number of rare species.
 
“The survey shows that the deforestation at Mtamba, Kola, Chakenge villages has disturbed these animals. Fire outbreak has also hurt the biodiversity at Kifuru and Kazimzumbwi,” said Gwegime.
For his part, Project manager, Elinas Monga said the survey results indicate that in 2003, there was a slight decrease of forest disturbances compared to 2011.
 
The researchers urged the village natural resource Committee (VNRC’s), village chairmen, foresters, Tanzania and Forest Service (TFS) to make sure that they commit themselves to protect and manage the forest reserve.

Wednesday, January 28, 2015



Askari wa Zimamoto wakiendelea na jitihada za kumaliza kuzima  moto Uliounguza Club Olympia Sinza


nnnnnnn


TAARIFA KAMILI YA KUKAMATWA PROFESA LIPUMBA NA POLISI
By: Julius Mtatiro,
27 Januari 2015,
Masomoni.

 Profesa Lipumba na Manaibu Wakurugenzi wawili wa Chama Cha Wananchi CUF (Shaweji Mketo na Abdul Kambaya), pamoja na walinzi wa Profesa Lipumba, wamekamatwa na polisi. Pia, nimeongea na mhe. Joram Bashange, Mkurugenzi wa Fedha wa CUF, tayari yuko Central Police lakini hajaruhusiwa kuwaona viongozi. Mawakili wa CUF wanaelekea polisi pia.
KUMBUKIZI YA MWAKA 2001

Ukamataji huo uliotumia nguvu kubwa umetokea leo majira ya Mchana wilayani Temeke. Leo ni Januari 27 na ni siku yenye kumbukumbu muhimu kwa Chama Cha Wananchi CUF baada ya matukio ya mauaji yaliyofanyika tarehe na mwezi kama huu huko Zanzibar ambako wafuasi wa CUF zaidi ya 100 waliuawa kwa risasi na vyombo vya dola. Mauaji hayo yalifuatiwa na maandamano mbalimbali yakiwemo ya Dar Es Salaam yaliyoongozwa na Prof. Lipumba ambaye alivunjwa mkono, kuporwa saa yake ya thamani na polisi, kukamatwa na kufunguliwa mashtaka.

MAANDAMANO YA CUF KILA MWAKA:
Baada ya tukio hilo CUF imekuwa na utaratibu wa kuandamana kila mwaka (maandamano ya amani) ili kuwakumbuka wahanga wa mauaji ya Januari 2001 na kuwaenzi waliopata ulemavu wa kudumu kutokana na kipigo cha vyombo vya dola. Mwaka jana 2014 mwezi kama huu Bendera za Chama cha Wananchi CUF zilipepea nusu mlingoti na pia maandamano yalifanywa maeneo kadhaa ya nchi na vyombo vya dola viliyalinda.

Mwaka huu nimeambiwa kuwa CUF ililijulisha jeshi la polisi juu ya maandamano ya leo kupitia barua ya Alhamisi, Tarehe 22 Januari 2014. Baada ya CUF kuandika barua hiyo, maandalizi ya maandamano na mkutano wa hadhara yaliendelea, ikiwemo kufanya matangazo kwenye wilaya za DSM, kukodi vifaa mbalimbali na hata kulipia matangazo LIVE kwenye redio kadhaa ili hotuba za viongozi ziweze kurushwa. Jeshi la polisi lilipokea barua hiyo tokea tarehe 22 Januari na likakaa kimya muda wote huo.
ZUIO LA POLISI:

Leo tarehe 27 Januari, maandamano yalipangwa kuanza saa 8 mchana kuanzia Temeke Mwisho kwenda hadi viwanja vya MBAGALA ZAKIEM ambako mkutano wa hadhara ungefanyika kuanzia saa 10.00 - 12.00 jioni. Cha ajabu ni kuwa, asubuhi ya leo ndipo Jeshi la Polisi limepeleka barua kwenye Ofisi Kuu za CUF Buguruni KUZUIA MAANDAMANO na MKUTANO WA HADHARA.

Barua hiyo iliyosainiwa na Kaimu Kamishna wa Polisi Kanda ya Dar Es Salaam na Pwani inaeleza sababu kadhaa za zuio hilo:
1. Kwamba, maandamano ya CUF ya Mwezi Januari 2001 yaliyofanya vyombo vya dola vitumie nguvu na kuua raia hayakuwa halali na hivyo kuadhimisha siku hiyo mwaka huu ni haramu na kunaweza kuhatarisha amani ya nchi.
2. Kwamba, Taarifa za kiintelijensia zinaonesha ati kuna watu wamepanga kufanya vurugu katika maandamano na mkutano huo.
3. Kwamba, kuna vitisho vya UGAIDI katika nchi yetu na hivyo maandamano hayo na mkutano huo vinaweza kuleta madhara ya magaidi kupenya na kutekeleza azma zao mbaya.
4. Sababu nyingine za kipuuzi, dhaifu na zisizo na maana.
Baada ya kupokea barua hiyo na kwa sababu wananchi na wapenzi wa CUF walikwishajikusanya kwa maelfu kwa ajili ya maandamano, ilimpasa Profesa Lipumba na viongozi waandamizi wa chama waweze kwenda hadi Temeke Mwisho ili kuahirisha maandamano hayo.
TEMEKE MWISHO:

Majira ya mchana leo, Profesa Lipumba aliongea na wanachama na wapenzi wa CUF waliojazana Temeke Mwisho karibu na Ofisi za CUF Wilaya na akaahirisha maandamano na mkutano (Usalama wa Taifa walikuwepo, Polisi walikuwepo kwa mamia na vyombo vya habari vilikuwepo). Baada ya kufanikiwa kuwatawanya wafuasi waliokuwa Temeke Mwisho, Profesa akajulishwa kuwa kule uwanjani Zakiem tayari kuna maelfu ya wafuasi, ikampasa yeye na viongozi waandamizi waingie katika magari na kuanza safari kwenda Zakiem kwa lengo la kuwatawanya wafuasi kwa amani kama alivyofanya kwa wale waliokusanyika Temeke Mwisho. Hapakuwa na wafuasi wa chama waliomfuata.

KUELEKEA MBAGALA ZAKIEM:

Wakiwa katika Magari yao na katika safari ya kwenda Mbagala Zakiem, wakazuiwa na magari zaidi ya 10 ya polisi walio tayari kwa mapambano. Profesa na viongozi wakawajulisha Polisi azma yao ya kwenda kutawanya wafuasi walioko Zakiem, baada ya mvutano mfupi Polisi hao waliwaruhusu waende Zakiem. Safari ya magari machache ikaendelea, bila wafuasi wanaotembea kwa miguu.

Walipofika mbele (Mtoni Mtongani - Round about) wakakuta BLOCK ya pili ya mamia ya Polisi wenye magari na silaha. Hawa nao wakawazuia wasiende ZAKIEM, wakati bado Profesa anawaelewesha, mabomu yakaanza kupigwa na viongozi kusambaratishwa kwa nguvu mno kama vile kulikuwa na jambo kubwa. Profesa amebebwa mzobemzobe akipigwa virungu na kutupwa kwenye DIFENDA ya polisi yeye, wakurugenzi wake na walinzi wake. Hivi sasa tuongeavyo wako CENTRAL POLICE na mie nilitoka tu kidogo Darasani ili kupiga simu na kusimuliwa tukio zima.
CHA KUSHANGAZA:

Wakati polisi wanazuia maandamano ya CUF kwa nguvu kubwa kiasi hiki, wanawapiga na kuwajeruhi viongozi wasio na hatia na ambao wamejishusha na kuahirisha maandamano na mkutano wao, Polisi haohao kila siku tunaona wanasimamia maandamano na mikutano ya Mwigulu Nchemba, Abdulrahman Kinana, Nape Nauye na viongozi chungu mbovu wa CCM.

Hata katika maadhimisho ya miaka 38 ya CCM yanayotarajiwa kufanyika mkoani Ruvuma, nimejulishwa kuwa kuna maandamano yamepangwa yakihusisha wana CCM mbalimbali katika wilaya za jirani ili kusheherekea sikukuu yao na kwamba Polisi watayalinda maandamano hayo ya CCM.
MASWALI YA KUJIULIZA:

Je, hizi taarifa za Kiintelijensia zinafanya kazi kwa mikutano na maandamano ya vyama vya upinzani tu? Je, hao Magaidi wao wanavamia na kulipua mikutano ya vyama vya upinzani tu? Magaidi gani hawa ambao hawaendi kuvamia wezi wa fedha za umma ati wanakwenda kuvamia viongozi waadilifu wanaopigania haki sawa kwa wote na mabadiliko makubwa katika nchi yetu? Tunadhani matendo haya ya serikali na vyombo vyake dhidi ya vyama vya upinzani yanajenga mustakabali wa taifa? Yanajenga amani na upendo miongoni mwetu? Au yanazidisha chuki na uhasama na mgawanyiko/mpasuko katika taifa?

Kwa nini mamia ya askari wanaokwenda kupiga na kujeruhi viongozi wenye nia njema yasitumike kwenda kusaka majambazi walioua askari wetu pale Ikwiriri Rufiji? Kwa nini mamia ya askari hao yasiwasake majambazi walioteka mabasi ya abiria mkoani Arusha majuzi? Kwa nini mamia ya Askari hao yasijielekeze kuwasaka wauaji wa Albino na wazee wenye macho mekundu Shinyanga?
Kwa nini mamia ya askari hao wasipelekwe kuwasaka magaidi ambao tumegundua watakuja kutuvamia? Na mbona maguvu hayo ya polisi yasielekezwe kuwasaka wala rushwa wakubwa, wafadhili na wamiliki wa mitandao ya kuuza madawa ya kulevya, wezi wa fedha za umma na waharibifu wakuu wa Taifa hili?
Mbona taifa hili linaendeshwa kipuuzi namna hii? Mbona nchi yetu inapelekwa mbele kama vile kuwa Chama Cha Upinzani ni dhambi dhidi ya watawala wezi na mafisadi? Kwa nini basi CCM hao hao wakapigia debe kuanzishwe vyama vingi mwaka 1992? Sasa wanaogopa na kuweweseka kwa lipi?
(UKIONA SERIKALI INAOGOPA MAANDAMANO YA AMANI NA MKUTANO WA CHAMA KIMOJA TU HADI KUPIGA NA KUKAMATA VIONGOZI, JUA KWAMBA SERIKALI HIYO HAINA SIKU NYINGI MADARAKANI).

"Time will determine and judge each of us".

Julius Mtatiro,
27 Januari 2015,
Masomoni.
MWENYEKITI WA CUF PROFESSA IBRAHIM LUPUMBA AKAMATWA

Uzinduzi wa ujenzi wa barabara za Mbezi mwisho-Goba-Tangi Bovu, Barabara ya External –Kilungule, Barabara ya Msewe-Baruti! Hii ni moja ya hatua kubwa sana na muhimu katika utatuzi wa foleni ndani ya Jiji la Dar es Salaam na kuendeleza kwa kiasi kikubwa maeneo ambayo barabara hizo zinapita (ndani ya Jimbo la Ubungo).